Wikiversity
Yaliyomo
Mandhari
Tarehe 14 Februari ni siku ya arubaini na tano ya mwaka. Mpaka uishe zinabaki siku 320 (321 katika miaka mirefu).
Matukio
- 1130 - Uchaguzi wa Papa Innocent II
Waliozaliwa
- 1861 - Andrew C. McLaughlin, mwanahistoria kutoka Marekani
- 1869 - Charles Wilson, mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia mwaka wa 1927
- 1917 - Herbert Hauptman, mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia mwaka wa 1985
Waliofariki
- 869 - Mt. Kyrilo, mmonaki kutoka Ugiriki ambaye alieneza Ukristo kati ya Waslavoni pamoja na mdogo wake Mt. Methodi na kubuni mwandiko wa Kikyrili
- 1779 - James Cook, mpelelezi kutoka Uingereza
- 1975 - Julian Huxley, mwanabiolojia, na mkurugenzi wa kwanza wa UNESCO
- 1975 - P. G. Wodehouse, mwandishi kutoka Uingereza
- 1982 - Antonio Casas, mwigizaji wa filamu kutoka Hispania
- 2015 - Philip Levine, mshairi kutoka Marekani
Sikukuu
- Wakristo wengi, wakifuata mapokeo ya Roma, huadhimisha kumbukumbu za watakatifu Sirili wa Thesalonike na Methodi wa Thesalonike, Valentinus, Vitalis wa Spoleto, Zeno wa Roma, Basiano na wenzake, Eleukadio, Ausenti abati, Nostriano, Antonino wa Sorrento, Yohane Mbatizaji Garcia n.k.
- Kutokana na sikukuu ya mtakatifu Valentinus, tarehe hii inasheherekewa kama "Siku ya wapendanao"
Viungo vya nje
- BBC: On This Day Archived 18 Februari 2007 at the Wayback Machine.