Statistical Genetics Wiki
Uhaini (kutoka neno la Kiarabu) ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kutoa habari za siri.
Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria na adhabu tofauti dhidi ya matendo ya kihaini, hata adhabu ya kifo.
Miongoni mwa wahaini maarufu duniani kuna Yuda Iskarioti, Benedict Arnold, Philippe Pétain na Vidkun Quisling.