Type a search term to find related articles by LIMS subject matter experts gathered from the most trusted and dynamic collaboration tools in the laboratory informatics industry.
| |||
Lugha ya taifa | Kireno | ||
Mji Mkuu | Maputo | ||
Aina ya Serikali | Jamhuri | ||
Rais | Filipe Nyusi | ||
Waziri Mkuu | Adriano Maleiane | ||
Eneo | km² 801.590 | ||
Wakazi | 31,693,239 (Julai 2022) | ||
Wakazi kwa km² | 28.7 | ||
JPT/ Mkazi | 233 US-$ (2004) | ||
Uhuru | kutoka Ureno tar. 25 June 1975 | ||
Pesa | Metical (MZM) | ||
Wakati | UTC +2h | ||
Wimbo wa Taifa | Pátria Amada (kwa Kireno: Nchi pendwa) | ||
Namba ya simu ya kimataifa | +258 | ||
Msumbiji (kwa Kireno: Moçambique) ni nchi ya Afrika ya Kusini-Mashariki.
Msumbiji iko ufukoni mwa Bahari Hindi ikipakana na Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Eswatini.
Upande wa mashariki kuna kisiwa cha Madagaska ng'ambo ya mlango bahari wa Msumbiji.
Jina la nchi limetokana na Kisiwa cha Msumbiji (kwa Kireno: Ilha de Moçambique) kilichokuwa boma na makao makuu ya Ureno kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki.
Sikukuu ya Taifa ni tarehe 25 Juni, ulipopatikana na uhuru mwaka 1975.
Tambarare ya pwani ni sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, lakini kwenda kaskazini upana wake unapungua.
Nyuma ya tambarare nchi inapanda hadi kufika uwiano wa tambarare ya juu ya Afrika ya Kusini.
Milima mirefu zaidi inajulikana kama Inyanga yenye mita 2500 juu ya UB: iko katika jimbo la Tete inayopakana na Zimbabwe, Zambia na Malawi.
Mito iko mingi, mkubwa zaidi ukiwa ndio Zambezi, halafu Ruvuma mpakani kwa Tanzania, Save na Limpopo.
Ziwa la Nyassa ni sehemu ya mpaka na Malawi.
Umbo la eneo la nchi ni refu sana: ni kilomita 2000 kutoka mpaka wa Tanzania upande wa kaskazini hadi Maputo iliyoko karibu na Uswazi na Afrika Kusini.
Pwani ya Bahari Hindi ina urefu wa km 2.470.
Miji mikubwa zaidi ni Maputo (wakazi 1.191.613), Matola (wakazi 543.907) na Beira (wakazi 530.706).
Wakazi wa kwanza wa Msumbiji huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.
Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi ambao walimeza wakazi wa kwanza inavyothibitishwa na DNA.
Haijulikani ni lini ya kwamba wafanyabiashara Waarabu walianza kufika ufukoni na kujenga vituo na miji yao. Lakini utamaduni wa Waswahili ulifika hadi sehemu za mwambao wa Msumbiji. Hadi leo aina ya Kiswahili inazungumzwa kwenye visiwa vya Kirimba.
Mto wa Zambezi ilitumika kama njia ya mawasiliano na biashara kati ya Ufalme wa Mwene Mtapa (Zimbabwe) na wafanyabiashara wa pwani.
Taarifa za kimaandishi zinaanza na kufika kwa Wareno. Mwaka 1498 Vasco da Gama alifika akiwa njiani kuelekea Bara Hindi.
Baadaye Msumbiji ikawa koloni la Wareno hadi mwaka 1975 vita vya ukombozi vya miaka 1964-1974 vilipomalizika kwa ushindi.
Hata hivyo vilifuata vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka 1977-1992.
Nchini Msumbiji kuna makabila mengi sana, kama vile Wamakua, Wanyungwe, Wayao, Wamakonde na Watsonga.
Kila kabila lina lugha yake, lakini lugha rasmi ni Kireno, ambacho kinaweza kuzungumzwa na 50.3% za wakazi, ingawa ni lugha ya nyumbani kwa 16.6% tu.
Upande wa dini, sensa ya mwaka 2017 ilikuta 59.2% ni Wakristo (hasa Waprotestanti na Wakatoliki, ambao ni 28.4%) na 18.9% ni Waislamu. 7.3% wanafuata dini asilia za Kiafrika au nyingine. Kumbe 13.9% hawana dini yoyote, kufuatana na kampeni ya Ukomunisti ya miaka 1979-1982.
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Msumbiji kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa . |