Effects of the storage conditions on the stability of natural and synthetic cannabis in biological matrices for forensic toxicology analysis: An update from the literature
Yaliyomo
![](https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b1/Maya_Yoshida.jpg/200px-Maya_Yoshida.jpg)
Maya Yoshida (Kijapani:吉田 麻也, alizaliwa tarehe 24 Agosti mwaka 1988) ni mchezaji wa soka wa Japani ambaye hucheza katika klabu ya Southampton Ligi kuu ya Uingereza na timu ya taifa ya Japan.
Nagoya Grampus
Alizaliwa Nagasaki, Yoshida alikuwa mchezaji wa kujihami wakati akicheza timu ya vijana ya Grampus, Katika msimu wa 2008, alikuwa katika kikosi cha kwanza. Alifanikisha Nagoya Grampus katika Ligi ya Mabingwa ya AFC katika mchezo dhidi ya Ulsan Hyundai Horang- tarehe 10 Machi 2009.
VVV-Venlo
Desemba 2009,ilitangazwa kwamba Yoshida alikuwa amehamishiwa kwenye klabu ya nchini Uholanzi iitwayo VVV-Venlo. Alipenda kucheza katika klabu za huko Ulaya tangu alipokuwa mdogo.Hakika,Yoshida alifuata hatua za Keisuke Honda ambaye pia alicheza VVV-Venlo kabla ya kujiunga nao.
Southampton
Mnamo tarehe 30 Agosti mwaka 2012, alikubali kujiunga na Southampton kwenye mkataba wa miaka mitatu kwa ada ya £ 3,000,000.i
Tarehe 9 Agosti mwaka 2013,ilitangazwa kuwa Yoshida atakuwa kwenye kikosi cha Toleo la kwanza la timu ya taifa ya japani katika mashindao ya FIFA.
Mnamo Januari 2015 Southampton ilitangaza kuwa Yoshida wamekubaliana na klabu na kuongeza mkataba wake hadi mwaka 2018.
Takwimu
Timu ya Taifa ya Japani | ||
---|---|---|
Mwaka | Mechi | Magoli |
2010 | 1 | 0 |
2011 | 12 | 2 |
2012 | 9 | 0 |
2013 | 15 | 0 |
2014 | 11 | 1 |
2015 | 13 | 3 |
2016 | 10 | 3 |
2017 | 9 | 1 |
2018 | 9 | 0 |
2019 | 11 | 1 |
Jumla | 100 | 11 |
Tanbihi
- ↑ Maya Yoshida at National-Football-Teams.com